Wednesday, February 12, 2020

TIBA YA KIFUA NA PUMU HATA KAMA NI SUGU.
chukua binzari shomari, mdalasini, a rkisusi, habbat Sauda, zaatar, khaulinjan na lisaan uswfuur, ziponde kisha ziloweke kwenye maji Lita moja na nusu ichemshe mpaka ibaki Lita moja

Matumizi
Mtoto mchanga kijiko cha chai Mara 3, mtoto wa mwaka 1-3 kijiko cha chakula Mara 3, mtoto miaka 8-12 kikombe cha kahawa Mara 3, waliojuu ya miaka 12 robo kikombe cha chain. Kwa mda wa siku 21.       
 DAWA YA MAFUA ISIYO NA MADHARA

Watu wengi husumbuliwa sana na mafua makali na wakati mwingine kupiga chafya mfululizo.

 Ili kuondokana na tatizo la mafua unashauriwa kuandaa kinywaji kifuatacho kisicho na kemikali.

MAANDALIZI

Chukua :

1. Maji lita moja

2. Asali vijiko 3 vikubwa vya chakula

3. Tangawizi ya unga kijiko kimoja kikubwa cha chakula au tangawizi mbichi itwange upate mchanganyiko uliopondeka kijiko kimoja kilichojaa.

Chemsha mchangyanyiko wako wote huo kwa pamoja mpaka uchemke vizuri ambapo inategemea na moto wa jiko lako lakini mpaka utakapoona imechemka vizuri usiache ikakaukia jikoni inashauriwa dakika 15 hadi 20 inatosha.

Kisha iache ipoe na KUNYWA NUSU GLASI MARA TATU kwa siku yaani asubuhi , mchana na usiku.

 Kwa wale walio na mafua sugu yanadondoka muda wote na kupiga chafya nyingi sana zisizo na idadi basi zitakata mara moja na siku ya pili zitaisha kabisa kumbuka kunywa dawa hii mwezi mzima au hadi miezi miwili utapona kabisa.

Kinywaji hiki ni dawa ya mafua safi kabisa unatumia siku moja tu unakua na nafuu kabisa ila dozi yake inataka utumie mwezi mmoja hadi mwezi mmoja na nusu mfululizo bila ya kuacha.
Hata ukiona umepoa endelea kutumia kwani Hii ni itakusaidia hata kwa maradhi mengine na kuepuka mafua kuja mara kwa mara

Sunday, October 27, 2019

TIBA YA KUFUNGA/KUFUNGUA  HEDHI

Kwa mwanamke  ambaye anapata tatizo katika siku zake ama kuzidi siku au kutopata siku atumie tiba mojawapo  Kati ya zifuatazo in Shaa Allah atakaa vema.

   DAWA YA KWANZA

MDALASINI; Kama ni unga, weka kijiko kimoja kwenye uji/chai/maji moto kutwa mara mbili kwa siku Saba

DAWA YAPILI

MVUJE &PILIPILI MTAMA; Chemsha vyote kwa pamoja kisha uwe unakunnywa kikombe cha kahawa kutwa mara mbili kwa siku saba 

DAWA YA TATU

KITUNGUU MAJI; Tengeneza juisi yake kisha kunywa kikombe kimoja cha kikombe cha kahawa kutwa mara mbili  kwa muda wa siku  TATU.

DAWA YA NNE 

ZAATAR; Chukua vijiko vitano vya dawa hii kisha chemsha kwenye maji ya lita mbili kiasi cha kupungua nusu lita na kubaki lita moja na nusu, kunywa kikombe cha kahawa kutwa mara mbili kwa siku tano 

Kwa MAELEZO zaidi wasiliana na mwl. NAHONYO F.M 
SIMU; 0712829903/0784950236

EMAIL; fnahonyo@gmail.com
BLOG; www.nahonyo.blogspot.com

Thursday, January 10, 2019

TIBA RAHISI KWA HEDHI ISIYOKOMA

Pata mizizi ya kutosha ya mbaazi kisha katakata ndimu vipande vipande bila kumenya, changanya na mizizi hiyo ya m'baazi na tia maji kiasi, chemsha kama chai kisha ipua. Kunywa kikombe kimoja cha chai asubuhi na jioni kila siku kwa siku saba inshaallah hedhi itakoma na etaenda kama kawaida.

KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NAMI MWL. NAHONYO
SIMU; 0712829903/0784950236/0762194681
EMAIL; fnahonyo@gmail.com AU TEMBELEA

Thursday, November 22, 2018

NUFAIKA NA TIBA ZETU

Jifunze jinsi ya kujitibu maradhi ya magonjwa mbalimbali kwa kutumia miti na Qur-an tukufu kupitia application ya Tiba

Download Tiba App kupata mafunzo
Bonyeza hapa https://play.google.com/store/apps/details?id=com.kimenya.treatments
 usisahau kutuma kwa watu wengine ili nao wanufaike 

Monday, August 22, 2016

TAFAKARI YANGU

Amani ndio msingi wa Maendeleo. Amani ikitoweka kuirudisha ni vigumu kabisa, Kama amani ikitoweka hakuna kinachowezakufanyika katika nyanja zote za maisha, hakuna kulima, kusoma, kucheza, siasa, kusafiri, utamaduni wala ibada. Ombi langu Watanzania wenzangu nikuwa tutunze amani tuliyonayo zaidi ya mboni ya jicho letu. Kila mmoja kwa nafasi yake afanye afanyalo kwa kufuata katiba ya nchi  huku akijua ameshikiria yai la amani. 

TAFAKARI YANGU

Amani ndio msingi wa Maendeleo. Amani ikitoweka kuurudisha ni vigumu kabisa, Kama amani ikitoweka hakuna kinachowezakufanyika katika nyanja zote za maisha, hakuna kulima, kusoma, kucheza, siasa, kusafiri, utamaduni wala ibada. Ombi langu Watanzania wenzangu nikuwa tutunze amani tuliyonayo zaidi ya mboni ya jicho letu. Kila mmoja kwa nafasi yake afanye afanyalo kwa kufuata katiba ya nchi  huku akijua ameshikiria yai la amani.