Friday, December 9, 2011

SALAMU ZA NDOA SEHEMU 1

         Shukrani zisizo  na  kikomo  ni  zake Allah, Muumba  na  mlinzi  wa  viumbe  wote. Rehema  na  amani  zishuke  kwake Mtume Muhammad(s.a.w) na watu  wake  wote pamoja  na  maswahaba  wake.

         Ndoa  ni lazima/wajibu kwa mtu ambaye  hawezi  kujizuia  na  ZINAA na  akawa  ni  mwenye  uwezo  juu  ya  MAHARI  na matumizi (mahitaj /huduma)  kwa mke. Katika  ndoa MAHARI ni  kitu  cha lazima  kwa jina  jingine  huitwa  SADAKA, hii  ni mali  anayotoa  mume  kumpa mke  na wala  si  wazazi  au jamaa wa mke  bali  ni  yake  mwenyewe  mwanamke. Lakini  mke  anaweza  kuamua  kwa  hisani  yake  mwenyewe  kuwapa  wazazi  wake  au  kwenda  kutumia  na  mume  wake.  Wazazi  na  jamaa  kupanga  kiasi  cha  MAHARI  na  kutumia  bila  kumshirikisha binti  mwenyewe  ni  makosa  makubwa  ndugu  zangu.

         Makosa  mengine  tunayofanya ni  kutoza  MAHARI  kubwa,  jambo  hili  linapelekea  wanaume  waliowengi  washindwe  kuona  kwasababu  ya  kukosa  uwezo  na  hatimaye  wanaendelea  na  maasi  ya  ZINAA  na  wale  wanaobahatika kuoa  kwa MAHARI  hiyo  kubwa  wanabaki  hata  hawana  kianzio  katika  maisha  yao  ya  ndoa. MAHARI haina kikomo/ mpaka kwa uchache au wingi wake lakini kinacho takiwa MAHARI hiyo iwe na manufaa na thamani , Mtume (S.A;W) juu ya hili anasema "TOENI ANGALAU PETE YA CHUMA"

         Katika kuchumbia ni  SUNNA   kwa  mume kutazama  uso  na  viganja  vya  mchumba  wake na wakati wa kutazama awapo ndungu wa mke, juu la hili mtume anasema "ATAKAPOCHUMBIA MMOJA WENU MWANAMKE AKIWEZA KUYATAZAMA YALE YATAKAYO MPELEKEA KUMUOWA KWAKE BASI AFANYE". Hapa tunaambiwa  kutazama  uso na viganja  vyake  na wala  si  kufanya  nae  ZINAA  ati tunafanya majaribio (practical ) majaribio. kufanya hivyo kabla ya ndoa ni makosa makubwa na hukumu yake ni kuchapa BAKORA MIA (100). kwa Mume na Mke, kwa vile ni wazinifu.
       
       Ndoa ya kiislam ili iswihi /ikubalike ni lazima  awepo Mlezi /Msaidizi na mashahidi wawili waislamu waliowaadilifu, Waliohuru na wawe wanaume (kwa pande zote mbili ). Juu ya hili Mtume  (S.A.W) anasema MASHAIDI WAADILIFU". Sasa je, Ndoa hizo za mkeka hao wote wanakuwepo? kama wanakosekana uhalali unatoka wapi?
     
       Enyi ndugu zangu, ni haramu /haitakiwi kwa muislamu kumuoa au kuolewa na asiye kuwa muislamu na vilevile ni haramu kuolewa au kumuoa ndugu yako kwa ukaribu wa ukoo au KUNYONYA au UKWE au kuwachanganya ndugu pamoja (yaani mkumbwa na mdogo au mapacha kuwaoa wote kwa pamoja kama wafanyavyo wengine).

     Enyi ndugu zangu mliokili upweke na utukufu wa Allah, hivi jinsi tunavyosherekea ndoa zetu ndivyo inavyotakiwa katika ndoa, tunaweka Mikesha ambayo inaambatana na muziki na pengine na pombe. jamani ndiyo ni furaha lakini mnaonaje furaha hiyo tujisherekea kwa kusoma Quran, kupeana mawaidha, kusoma riwaya za Mtume (S.A.W). kuburudika kwa Qaswida na pengine hata kwa Dhiki?.
     
     Kumbuka: "MJNGA NCHI NI MWANANCHI" na "MJENGA DINI NI MWANADINI (MUUMINI)". Kwa hiyo basi tufanye mambo yanayoendeleza dini na wala si yale yanayopunguza thamani ya dini. Ndoa ni jambo la furaha na Kheri kwa hiyo tutumie nafasi hiyo kuomba dua ili Allah alete mafanikio katika ndoa badala ya kuweka kanda za muziki tuweke kanda za dini. tuzinduke zangu ili tufanikiwe hapa Duiniani na kesho Akhera.

     Kwa leo namalizia kwa maneno ya kiongozi watu Mtume (S.A.W) pale aliposema "MTU MWENYE KUWEZA MIONGONI  MWENU KUOA BASI AOE HAKIKA LINASITIRI JICHO NA NI KINGA YA UTUPU NA ASIYEWEZA  (KUOA ) BASI NI JUU YAKE KUFUNGA"
"MWENYEZI MUNGU NA MTUME WAKE NDIO WANAOJUA KULIKO MIMI NA WEWE.            
                                     SALAMU HIZI ZIMETOLEWA NAMI MCHACHE WA ELIMU.
                                                                   MWL. NAHONYO  (FASANA)
                    

















NUFAIKA NA MAFUTA YA MISKI

Miski  ni  mama  wa  mafuta yote  mazuri  duniani. Kutokana  na  ubora  au  umuhimu  wake  katika  tiba na  manukato  watu  wengi wamekuwa  wakichakachua  na  kuzalisha  miski  feki.


UNAWEZAJE  KUTAMBUA  MISKI  FEKI  NA  HALISI?
 Unaweza  kutambua  kwa  kunusa,  kupima  uzito  na  ladha. Kwa  upande  wa   ladha,  miski  halisi  inakuwa  na  ladha  ya  uchungu  isiyochanganyika  na  sukari,  na  kama  utaonja  basi  utapata  msisimuko  fulani. Pia  kama  utayasomea Ruqia  na  kumpakaa  mgonjwa  wa  masheitani  athari  zake  huonekana  maramoja.



 MATUMIZI  YA  MAFUTA  YA  MISIKI  KAMA  TIBA 

 1. Ni  kinga  na  tiba  ya  masheitani  wa  kijini  na  kibinadamu.  MATUMIZI; Changanya  mafuta  ya  miski  na  ya  zaituni  halafu  uwe  unajipakaa mwilimzima asubuhi na jioni. ukkosa mafuta ya zaituni unaweza kutumia mafuta ya miski pekeyake.
2.Kusafisha na kufungua milango ya fahamu-MATUMIZI; Nusa marakwamara.

3.Kuongeza hamu ya chakula cha usiku kwa wanandoa. MATUMIZI; weka maji katika glasi halafu dondoshea matone matatu ya miski, halafu unywe na kujipaka sehemu nyeti dakika tano kabla ya kwenda chakulani. hii ni kwa wanaume na wanawake.

4. Kusafisha sehemu nyeti. MATUMIZI; Wanawake baada ya kumaliza siku zao wanaweza kutumia mafuta haya kwa kuondoa harufu, lakini pia kwa kuongeza ashiki (hamu). ONYO: Usitumiye bila kuchanganya na maji na usitumiye kama hauko katika ndoa nakama uko mbalimbali na mume wako.

5. Tiba ya uke ulio legea. MATUMIZI; Changanya na maji halafu uwe unanawa kwa ajili ya kukaza uke, kupunguza maji na kufanya sehemu hiyo kuwa ndogo.

6. Kipimo cha maradhi ya kijini. MATUMIZI; Pakaa matundu thelathini na mbili wakati wa usiku ambayo ni ncha za vidole, chuchu, macho, masikio, pua, mbeleni na nyumani. ukipakaa kama unasumbuliwa na jini basi utaummwa na kichwa au kupata mawengemawenge.

7.Tiba ya fangasi. MATUMIZI; Pakaa sehemu yenye fangasi marambli kwa siku, kwa muda wa siku saba Inshaallah utapona

Thursday, November 17, 2011

KILA MUISLAMU ANADHIMA YA KUENDELEZA UISALAMU.

Shukrani  zilizo takasika ni zake Allah (s.w.t) asiyekuwa na mshirika katika  Ibada yake  wala katika  ufalme  wake.
Rehema na Amani zishuke juu ya Mtume Muhammad (s.a.w) na wale wote wenye kushikamana naye.
Mwenyezi Mungu ametujaalia wanadamu kuwa makundi mbali mbali  kama vile  masikini  na  matajiri, wafanyakazi  na  wakulima  na  makundi  mengine  mengi. Pamoja na  kuwepo na  makundi  mbali mbali  kila  kundi  linatakiwa  kumcha  Allah (s.w.t) na kuwa mstari wa  mbele  katika  kuendeleza  dini.
Wewe na mimi  tumetamka shahada mbili  na tumekiri katika nyoyo zetu kuwa mwenye jina la Allah ndiye  Mungu wa  kweli  na Muhammad ni Mtume wake, Kukiri na kutamka shahada ni dalili tu ya kujulisha  kuwa sisi ni waislamu. Ili uislamu wetu uweze kukamilika  tunatakiwa  kuyafanya  yale ambayo wametuagiza Allah (s.w.t.) na Mtume wake (s.a.w) na kuyaacha yale ambayo wametukakaza.
Katika  makundi tuliyonayo wanadamu,  kundi la wafanya kazi huwa wamepitia  hatua mbalimbali kama vile shule ya msingi, sekondari, chuoni na  hatimaye kazini. Sasa ewe uliyejaaliwa kuajiriwa ujiulize  ukiwa shule  ya  msingi, sekondari na chuoni, mlianza wangapi, mlifaulu  wangapi na mpaka hivi sasa ni wangapi mnaendelea na kazi?
Je, wale ambao hawakufanikiwa katika yale maeneo ambayo wewe umefanikiwa unafikiri ni uzembe wao  au Allah hakuwawezesha? Na wewe uliyefanikiwa unafikiri umefanikiwa kwa ujanja wako au Allah ndiye aliyekuwezesha?
Allah (s.w.t) humpa amtakaye na humnyima amtakaye, umekuwa miongoni mwa waliopewa na Allah basi nawe utoe katika njia ya Allah ili kuendeleza dini yake si kwaajili ya kumnufaisha mwenyezi mungu bali ni kwaajili ya kutaka radhi ili aendelee kukuruzuku na kulinda  mali  yako.
Mwenyezi Mungu anatuhimiza kwa kusema ndani ya Quran: ENYI MLIOAMINI TOENI KATIKA VILE TULIVYOKUPENI KABLA HAIJAFIKA SIKU AMBAYO HAPATAKUWA (NA) KUJIKOMBOA WALA URAFIKI (WA KUSAIDIANA) WALA UOMBEZI, NA WALIOKUFURU NDIO WALIO JIDHULUMU (KWELIKWELI) Q:2:254.    
Allah (s.w.t.) ametuumba wanadamu akatupa uwezo kuliko viumbe wote, ametupa elimu, akatupa pia uhuru wa kuweza kupanga na kupangua,  kutanda na  kutandua, kufunga  na kufungua  na mengine  mengi.  Tujiulize  enyi wenzangu, katika kipato  chetu  tunatumia kiasi  gani  katika  mambo  ya anasa?
Kwanini tunakunja mikono yetu katika upande wa kundeleza dini yetu?
Sisi tuliojaaliwa kuwa na uhakika wa kipato  tena kwa muda maalumu tunakuwa wazito kutoa. Je, wale wasio kuwa na uhakika wa kipato kwa muda maalumu wataweza? Waislamu wenyewe tusipo iendeleza dini yetu asiye kuwa Muislamu ataweza kuundeleza Uislamu?
Allah (s.w.t) amemsifu binaadamu kwa kusema “ HAKIKA TUMEMUUMBA MWANAADAMU KATIKA UMBO LILILO BORA KABISA”Q 95:4. Hapa inamaana wewe na mimi tumejaliwa  vipawa  vinavyoweza kutuwezesha kutambua dhima ya kuumbwa kwetu na hatima ya maisha yetu hapa duniani na kesho akhera.
Enyi ndugu zangu katika imani na dinI  tujitahidi kutoa bila kuwa na mashaka ya kulipwa katika vile tunavyovitoa, Allah  ameahidi kumlipa kila  mtu kwa kila akifanyacho kiwe cha  kheri au shari, kidogo au kikubwa, akiwa ametoa kwa siri au wazi kama  anavyosema ndani ya Quran 2:274 “WALE WANAOTOA MALI  ZAO USIKU NA MCHANA KWA SIRI NA DHAHIRI, WANAUJIRA WAO KWA MOLA WAO, WALA HAITAKUWA KHOFU JUU YAO  WALA HAWATAHUZUNIKA”
Ewe Mwenyezi Mungu , kila atakaye kunjua  mkono wake na kutoa kwako basi mtengenezee mambo yake hapa Duniani na Kesho Akhera.

KILA MUISLAMU ANDHIMA YA KUENDELEZA UISALAMU.

Shukrani  zilizo takasika ni zake Allah (s.w.t) asiyekuwa na mshirika katika  Ibada yake  wala katika  ufalme  wake.
Rehema na Amani zishuke juu ya Mtume Muhammad (s.a.w) na wale wote wenye kushikamana naye.
Mwenyezi Mungu ametujaalia wanadamu kuwa makundi mbali mbali  kama vile  masikini  na  matajiri, wafanya  kazi  na  wakulima  na  makundi  mengine  mengi. Pamoja na  kuwepo na  makundi  mbali  mbali  kila  kundi  linatakiwa  kumcha  Allah (s.w.t) na kuwa msari wa  mbele  katika  kuendeleza  dini.
Wewe na mimi  tumetamka shahada mbili  na tumekirir katika nyoyo zetu kuwa mwenye jina la Allah ndiye  mungu wa  kweli  na Muhammad ni Mtume wake, kukiri na kutamka shahada ni dalili tu ya kujulisha  kuwa sisi ni waislamu. Ili uislamu wetu uweze kukamilika  tunatakiwa  kuyafanya  yale ametuagiza Allah (s.w.t.) na Mtume wake na kuyaacha yale ambayo wametukakaza.
Katika  makundi tuliyonayo wanadamu  kundi la wafanya  kazi huwa wamepitia  hatua mbali  mbali kama vile shule ya msingi, sekondari, chuoni na  hatimaye kazini. Sasa ewe uliye jaaliwa muajiriwa ujiulize  ukiwa shule  ya  msingi, sekondari na chuoni, mlianza wangapi, mlifaulu  wangapi na mpaka hivi sasa ni wa ngapi mnaendelea na kazi?
Je wale ambao hawaku fanikiwa katika yale maeneo ambayo wewe umefanikiwa unafikiri ni uzembe wao  au Allah hakuwawezesha? Na wew uliye fanikiwa unafikiri umefanikiwa kwa ujanja wako au Allah ndiye aliyekuwezesha?
Allah (s.w.t) humpa amtakaye na humnyima amtakaye, umekuwa miongoni mwa waliopewa na Allah basi nawe utowe katika njia ya Allah ili kuendeleza dini yake si kwaajili ya kumnufaisha mwenyezi mungu bali ni kwaajili ya kutaka radhi ili aendelee kukuruzuku na kulinda  mali  yako.
Mwenyezi Mungu anatuhimiza kwa kusema ndani ya Quran: ENYI MLIOAMINI TOENI KATIKA VILE TULIVYOKUPENI KABLA HAIJA FIKA SIKU AMBAYO HAPATAKUWA (NA) WALA URAFIKI (WA KUSAIDIANA) WALA UOMBEZI, NA WALIOKUFURU NDIO WALIO JIDHULUMU (KWELIKWELI) Q:2:254.    
Allah (s.w.t.) ametuambia wanadamu atatupa uwezo kuliko viumbe wote, ametupa elimu, akatupa pia uhuru wa kuweza kupanga na kupangua,  kutanda na  kutandua, kufunga  na kufungua  na mengine  mengi.  Tujiulize  enyi wenzangu, katika kipato  chetu  tunatumia kiasi  gani  katika  mabo  ya anasa?
Kwanini tunakunja mikono yetu katika upnde wa kundeleza dini yetu?
Sisi tuliojaaliwa kuwa na uhakika wa kupata tena kwa muda maalumu tunakuwa wazito wakutoa je, wale wasio kuwa na uhakika wa kipato kwa muda maalumu wataweza? Waislamu wenyewe tusipo iendeleza dini yetu asiye kuwa Muislamu ataweza kuundeleza Uislamu?
Allah (s.w.t) amemsifu binaadamu kwa kusema “ HAKIKA TUMEMUUMBA MWANAADAMU KATIKA UMBO LILILO BORA KABISA” 95:4. Hapa inamaana wewe na mimi tumejaliwa  vipawa  vinavyoweza kutuwezesha kutambua dhima ya kuumbwa kwetu na hatima ya maisha yetu hapa duniani na kesho akhera.
Enyi ndugu zangu katika imani na din tujitahidi kutoa bila kuwa na mashaka ya kulipwa katika vile tunavyovitoa, Allah  ameahidi kumlipa lika mtu kwa kila akifanyacho kiwe ch kheri au shari, kidogo au kikubwa, akiwa ametoa kwa siri au wazi kama navyo sema ndani ya Quran 2:274 “WALE WANAOTOA MALI ZAO USIKU NA MCHANA KWASIRI NA DHAHIRI, WANAUJIRA WAO KWA MOLA WAO, WALA HAITAKUWA KHOFU JUU YAO  WALA H WATA HUZUNIKA”
Ewe Mwenyezi Mungu , kila atakaye kunjua  mkono wake na kutoa kwako basi mtengenezee mambo yake hapa Duniani na Kesho Akhera.

SALAMU ZA NDOA SEHEMU YA (II)

Kila sifa njema ni  zake Allah (s.w.t) muumba wa viumbe wote. Rehema za mwenyezi Mungu zishuke kwa Mtume Muhammadi (s.a.w) na watu wake wote.
TALAKA ni halali lakini ni halali inayochukiza kwa mwenyezi Mungu kwa sababu ya maudhi na madhara yanayo patikana baada ya wanandoa kutengana. Juu ya hii Mtume (s.a.w) anasema “ JAMBO  LA HALALI KULIFANYA LAKINI LINACHUKIZA SANA MBELE YA MWENYEZI MUNGU (S.W.T) NI MTU KUTOA TALAKA (Yaani kumuacha mke)”
Watu wanapokuwa katika ndoa wajue kuwa wako katika vazi, rehema, upendo na amani, lakini wanapoachana mambo hayo yote hutoweka na kusababisha matatizo na maudhi na pengine hujiingiza katika  maovu, na kama walibahatika kupata watoto basi watakosa malezi ya wazazi wote kwa pamoja na hivyo kuwafanya wakose kujengewa msingi mzuri wa KIMAADILI.
Katika uislamu hatuna mafunzo yanayo wafanya watu watengane, bali mafunzo tuliyonayo ni yakuwasuluhisha watu wapatane, na jambo hili ni jukumu la kila aliye kiongozi kuhakikisha kuwa anawapatanisha watu  waliogombana. Mwanamke anaweza kupewa talaka kama atafanya makosa makubwa yaliyowazi, kuwa muasi katika dini au kwa sababu yeyote ya msingi ya kisheria. Lakini hatua hii iwe ni hatua ya mwisho baada ya kutanguliwa na hatua zingine za awali za upatanishi.
Waliowengi miongoni mwetu wanafikiri kuwa talaka ni lazima tu iandikwe kwenye karatasi. Talaka inaweza kuandikwa, katika karatasi au inaweza kutolewa kwa matamko tu kama vile, nimekuacha, uko huru, ondoka tu , si mke wangu n.k. itaswihi maadamu tu yametolewa maneno hayo kwa nia ya talaka.    
Talaka inawahusu wale walio funga ndoa kisheria. Ifahamike kuwa mtu asiandike au kuzungumza jambo la talaka akasema ati nilikiwa ninatania, utani wake hautakubaliwa kisheria.
Mume anaruhusiwa kumiliki talaka tatu (3) lakini cha ajabu ni kwamba utamuona mtu anamtolea mkewe talaka zaidi ya tatu (3) huo sio uislamu bali ni USHETANI. Na hairuhusiwi kuzitoa talaka kwa  pamoja, bali talaka hutolewa moja moja. Na talaka ya kwanza na yapili huitwa talaka REJEA, yaani mume anaruhusiwa kumjerea mke wake ndani ya EDA yake. Na kama EDA yake ikiisha hana ruhusa kumrejea bali kwa ndoa nyengine tena akitaka. Na talaka ya tatu inaitwa talaka ya BAYANA, na mwenye kumpa mke talaka tatu hana ruhusa ya kumrejea mpaka aolewe na mume mwingine na sheria hapa inasema mpaka afanye naye tendo la ndoa halafu amuache kisha akae EDA amalize ndipo atapata ruhusa ya kumuoa tena kama anataka.
EDA zimegawanyika namna mbili yaani eda ya mwanamke kufiwa na mumewe na EDA ya talaka. EDA ya mwanamke aliyefiwa na mume wake kama ni mjamzito basi EDA itaisha mara atakapojifungua na kama si mjamzito atakaa  kwa muda wa miezi minne (4) na siku kumi (10) na mwanamke mwenye kukaa EDA kwa ajili ya kupewa talaka  kama ni mjamzito naye EDA yake itaisha mara tu baada ya kujifungua  na kama hana ujauzito basi atakaa kwa muda wa miezi mitatu. Mwanamke aliyepewa talaka moja  ndiye anayezungumziwa hapa.
Mwanamke mwenye kukaa EDA asitolewe hapo katika nyumba na wala hana ruhusa ya kutoka mwenyewe isipokuwa  akileta mambo ya ouvu yaliyo wazi inaruhusiwa kumfukuza. Mke anapokaa EDA basi ni jukumu la mume kumpa huduma huyo mke aliyempa talaka, vilevile ni jukumu la jamaa wa mume kumhudumia  mke aliyefiwa na mume wake mpaka EDA itakapoisha.
Huduma inayozungumziwa hapa ni ile ya mahitaji ya msingi na wala siyo kufanya naye ZINAA.
Ama watu wengi wanauliza ati, kwa nini mke akae EDA na mume asikae EDA? Kwa kifupi ni kwamba mume ndiye mchunga wa mke kwa hiyo muda wa mke ambao anakaa EDA ni kumpa nafasi ajiangalie hali yake kama  anaujauzito au la vilevile kwa upande wa EDA ya talaka inakuwa ni nafasi ya kuwafanya waliotengana kuombana msamaha na hivyo kufungua ukurasa mpya.
Ewe Mwenyezi Mungu nakuomba umuongoze kila anayesoma ujumbe huu na umruzuku kila anayesambaza ujumbe huu na vilevile uwape nguvu na moyo waislamu wengine kufanya kazi kama hii angalau kutoa mwongozo au ukumbusho kwa wengine. Mungu akiendelea kuniwezesha kwa hali na mali sitachoka daima nanyi wasomaji naomba mniombee mafanikio katika kazi hii INSHAALAAH. 

Wednesday, September 7, 2011

Tuzingatie mafunzo ya mwezi wa ramadhani

Tuendelee kuyaenzi yote tuliyojifunza katika mwezi wa Ramadhani, kwani M WENYEZI MUNGU yupo wakati wote na hakuna anayejua siku ya kuondoka hapa duniani.

Wednesday, August 31, 2011

TUZINGATIE MAFUNZO YA MWEZI WA RAMADHANI Ndugu zangu wote mnaofuatilia blog yangu, natambua kuwa kuna waislamu na wasio waislamu lakini pamoja na utofauti wetu wa imani bado mafunzo ya Ramadhan yanatugusa wote. Ukarimu, upendo, umoja na mshikamano, kuhurumiana, kusaidiana, kuvumiliana, kuheshimiana pamoja na kufanya matendo mengine ya kiuchamungu ni baadhi ya mafunzo ya mwezi wa Ramadhan. Mwenyezi Mungu yupo wakati wote, halali wala hasinzii, haendi likizo wala hasafiri kwanini tusiendeleze mafunzo ya mwezi mtukufu? Hakuna mwenye uhakika lini ataondoka hapa duniani, unaweza kumuasi mola wako leo, kesho kabla hujatubia ukaondoka duniani, je! Utakuwa mgeni wa nani?aofuatilia blog yangu, natambua kuwa kuna waislamu na wasio waislamu lakini pamoja na utofauti wetu wa imani bado mafunzo ya Ramadhan yanatugusa wote. Ukarimu, upendo, umoja na mshikamano, kuhurumiana, kusaidiana, kuvumiliana, kuheshimiana pamoja na kufanya matendo mengine ya kiuchamungu ni baadhi ya mafunzo ya mwezi wa Ramadhan. Mwenyezi Mungu yupo wakati wote, halali wala hasinzii, haendi likizo wala hasafiri kwanini tusiendeleze mafunzo ya mwezi mtukufu? Hakuna mwenye uhakika lini ataondoka hapa duniani, unaweza kumuasi mola wako leo, kesho kabla hujatubia ukaondoka duniani, je! Utakuwa mgeni wa nani?

Wednesday, July 20, 2011

FAIDA YA MAJI YA ZAMDA

Maji haya yanafaida kubwa kwa KUTIBU aina zote za maumivu ya tumbo.

                      MATUMIZI
kunywa maji ya zamda kikombe kimoja cha kahawa kutwa mara tatu kwa muda wa siku saba hadi ishirini na moja.INSHAALLAH UTAPONA.

TIBA YA JINO

Mwenye kuhisi maumivu ya jino apate asali vijiko 5 na mdalasini kijiko  kimoja. Mchanganyiko huu utakuwa unapaka kwa nje usawa wa jino linalouma kutwa mara tatu.INSHAALLAH UTAPONA.

TIBA YA MAFUA

(1)Maji ya moto kikombe kimoja cha chai
(2)Asali kijiko kimoja cha chakula
(3)Unga wa mdalasini kijiko kimoja cha chakula

        MATUMIZI
Changanya pamoja halafu uwe unakunywa kutwa mara tatu. kila unapotaka kunywa utakuwa unachanganya wakati huohuo. Tumia dozi hii kwa muda wa siku saba hadi siku kumi na moja.Tiba hii hutibu hata mafua mazito(chronic) na yenye kuziba pua.INSHAALLAH UTAPONA

Saturday, July 16, 2011

TIBA YA KIFUA NA PUMU

Kama  unatatizo  la  kifua  au  pumu  unaweza  kujitibu  kwa  kutumia  dawa  zifuatazo:-

(1) Vijiko vitano  vya unga  wa rifaj
(2) Vijiko  vitano  vya  unga  wa  karafuu
(3) Vijiko  vitano  vya  unga  wa  mjafar
(4) Vijiko  vitano  vya  unga  wa  tangawizi
(5) Vijiko  vitano  vya  unga  wa  alqusus na
(6) Asali mbichi na safi lita  moja

                              NAMNA  YA  KUANDAA
Changanya  vyote  kwa  pamoja  halafu  ukoroge  kwa  muda  mrefu  mpaka  uhakikishe   imechanganyika  vizuri.

                              MATUMIZI
Kula  kijiko kimoja  cha  chakula asubuhi,  mchana  na  jioni  kwa  muda  wa  siku  kumi  na  moja  hadi  siku  ishirini  na  moja.  INSHAALLAH  UTAPONA

DAWA YA SAHANYOZA

Hii  ni  dawa  ya  kupaka  ambayo  kwa  uwezo  wake  Allah (S.W) INAUWEZO  WA  KUTIBU  MARADHI  MBALIMBALI KAMA  VILE:-

(1) Maumivu  ya  kichwa
(2) Maumivu  ya  mgongo
(3) Maumivu  ya  kiuno
(4) Maumivu  ya mikono
(5) Maumivu  ya miguu
(6) maumivu  ya  viungo
(7) Vidonda  vya  koo
(8) Kung'atwa  na mdudu  na
(9) Fangasi za nje  ya  mwili

DAWA HII NI MCHANGANYIKO  WA DAWA MBALIMBALI  KAMA  VILE; HALIMIT, ELKZAMDA, HABAT SAUDA, ZAITUN. N.K.

MATUMIZI; PAKA SEHEMU  YENYE  MAUMIVU  MARAMBILI  KWA  SIKU  yaani  ASUBUHI  NA  JIONI.

Saturday, July 2, 2011

FAIDIKA NA MAFUTA YA ZAITUNI.


               BISMILLAH  ARRAHMAN  ARRAHIIM      
                       NUFAIKA  NA  MAFUTA  YA  ZAITUNI

Anasema  Allah  (S.W)  KUHUSU  MAFUTA  YA  ZAITUNI:
“…….TUNGI  LILE  NI  KAMA NYOTA  INAYOMEREMETA, INAYOWASHWA KWA  MAFUTA  YANAYOTOKA  KATIKA  MTI  ULIOBARIKIWA  WA  MZAITUNI.  SI  WA  MASHARIKI  WALA  MAGHARIBI.  YANAKARIBIA  MAFUTA  YAKE  KUNG’AA  YENYEWE  INGAWA  MOTO  HAUJAYAGUSA-NURU  JUU  YA  NURU……”(QUR’AN 24:35)

      Mafuta  ya  zaituni  yana  manufaa  mengi  katika  mwili na maisha  ya  binadamu  kwa  ujumla  kama  ifuatavyo;

(1)Mafuta  ya  zaituni  hutibu  maumivu  ya  tumbo  kwa  kunywa  kijiko  1  mara  2 kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  7  hadi  siku 11  inshaallah.

(2)Mafuta  ya  zaituni  hutibu  masheitani  kwa  kusomea  kisomo  cha Ruqia,  mgonjwa  atajipaka  mwili  mzima  mara  moja  kwa  siku  pamoja  na  kutafuna  vitunguu  saumu  punje tatu  wakati wa  kulala  kwa  muda  wa  siku  arobaini  inshaallah.

(3)Mafuta  ya  zaituni ni kinga  ya  masheitani  wa  kijini  na  wa  kibinadamu  kwa  kujipaka  mwili  mzima  mara  moja  kwa  siku.

(4)Mafuta  ya  zaituni  hutibu  ugonjwa  wa  mafua  kwa  kupaka  kwenye  mwamba  wa  pua  na  ndani  ya  matundu  ya  pua  mara  tatu  kwa   siku.

(5)Tiba  ya  vidonda  vya  tumbo; Matumizi  ni  kutia  vijiko  2  vya  chakula  katika  uji    mara  mbili  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  90.

(6) Mafuta  ya  zaituni  hutumika  kama  huduma  ya  kwanza  kwa  aliyekunywa  sumu  kwa  kunywa,  na kwa mwenye  ganzi  au kiharusi hutumia  kwa  kuchua  asubuhi  na  jioni.

(7) Mafuta  ya  zaituni  hutumika katika  kuua  wadudu  wabaya  walioko  tumboni  kwanjia  ya kunywa  kijiko  kimoja mara  mbili  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  saba.

(8) Mafuta  ya  zaituni huongeza  nguvu  za  kiume  kwa kunywa  kijiko  kimoja  kwa  siku  pamoja  na kuuchua  uume  mafuta  yaliyochanganywa  na vitunguu swaumu  kwa  muda  wa  siku  saba  hadi  kumi  na  moja.

(9) Tiba ya ugonjwa  wa  kusahau: paka katika paji la uso kutwa marambili pamojana kunywa kijiko kimoja cha  chai mara moja kwa siku kwa muda wa siku 7 hadi  siku 11.

(10) Tiba ya degedege: hutumika kupakaa mwili mzima mafuta yaliosomewa ruqya, marambili kwa siku kwa muda wa siku 7 hadi  siku 21.

(11)Kukojoa kitandani: kupakaa mafuta ya zaitun mwili mzima kutwa marambili huku akilamba matone mawili kwa  muda  wa siku 7 hadi  siku 21.

 Kwa maelezo, ushauri na msada wasiliana na:  Mwalimu NAHONYO,
                        Muslim university of Morogoro
                           P.O.BOX 1031
      fakihimshamu@yahoo.comNahonyo.blogspot.com. 0712829903 or 0784950236
 

Thursday, June 23, 2011

Zijuwe dalili za jini mahaba

Jini mahaba ni jini mithili ya majini wengine. lakini jini huyu huwa ana dalili mbali mbali kama zifuatavyo:-
1. kuwa na wivu kupindukia
2.kupata maumivu ya kichwa cha upande
3.kutopenda kuowa au kuolewa
4.chuki ndani ya ndoa
5.kuwa na nyuzuru katika tendo la ndoa
6.kuota ndoto nyevu za mapenzi.

kwa maelezo zaidi jipatie kitabu kinacho itwa " TIBA MUJAARABU" na RUQYA ya SHERIA dhidi ya uchawi, kijicho na husda.