Wednesday, March 28, 2012

VIJANA WA LEO





Tukumbuke jamani leo hivi tunafanya ujeuri katika mgongo huu wa ardhi kwa vile ni mpana, kesho tutakapoingia katika tumbo la ardhi, hakika hatutakuwa na sehemu ya kukimbilia. Katika tumbo la ardhi ni matendo mema tu ndio yatakufanya uwe katika amani, kama hauna matendo mema basi misukosuko itakupata.

Kwa kweli vijana wa leo ni waajabu kabisa, yaani mtu anaweza kumuona mgonjwa wa UKIMWI, kusikia au kusoma kuhusu gojwa la UKIMWI, atafikiri na kujuta kwa muda ule, akitembea hatua moja kutoka sehemu ya tukio basi anasahau kila kitu. Vipi vijana tunashindwa kuzimiliki akili zetu na utashi wetu.
Leo viwanja vimejaa miba, miiba ambayo ikituchoma tutapata mateso ya kuumwa sana na kesho tutaadhibiwa na Mwenyenzi Mungu juu ya zinaa. Hakika leo hivi tujue fika alama za kiama zimekwisha dhihiri, kwa hiyo tufanye maandalizi ya kuiaga hii dunia. Maandalizi yenyewe ni kurejea kwa muumba wetu na kufuata hukumu zake.

Leo hivi vijana wa kiume wakiona sketi (msichana) inapita, utasikia minong’ono. Wengine watasema angalia mzigo, wengine watasema angalia bonge la mlima au kiuno angalia demu na sifa nyingine watazitoa. Vijana wakike nao wakimuona mvulana au suruali anapita utasikia wakisema cheki buzi, kifaa, kidume, meni na mengineyo, maneno haya yote yanaonesha jinsi gani vijana tulivyotawaliwa na ibilisi.

Vijana hivi leo tunapokutana katika jumuiya mbalimbali kama katika vyuo, sekondari, na mikusanyiko mingine tukawa jinsi tofauti  basi kila mmoja atakuwa na tamaa ya kuwa na mpenzi. Jambo hili ni hatari sana kwa maisha yetu, maisha ya hapa duniani na kesho Akhera.

Hatari hapa duniani kwa vile  huwa tunachanganya suala la masomo na mapenzi, mapenzi yanaweza kutupotezea muda, mapenzi yanaweza kutufanya tuwe maskini kwa vile ndani yamapenzi ni vitu vya gharama ndivyo hutawala. Sivyo hivyo tu bali suala la magonjwa yazinaa hasahasa huyu muuaji wa furaha (A killer of joy) UKIMWI.

Ndugu zangu  hakuna njia ya mkato ya kuepukana  na huyu muuaji wa furaha (A killer of joy) bali ni kurejea kwa mola wetu. Tukirejea kwa mola wetu hakika tutafanya yale aliyo tuamrisha na kuacha yale aliyoyakemea. Kwa kufanya hivyo ndio amani kwetu. Kwa hiyo tukiendeleza zinaa tutateseka duniani na kesho akhera tutateseka.

Vijana wezangu hebu tujiulize tunapokutana katika jumuiya mbalimbali na kuwa na tama ya kuwa na mpenzi. Je kila mmoja anamjua mwenzake , anajua alikotoka ana tabia gani, je anakuwa na uhakika gani kuwa yuko salama, je anakuwa anavunja amri ya mungu   ya sita, inatuonya tusizini? Je tunaipinga ile aya inayotukataza tusikaribie zinaa.KUMBUKA EWE NDUGU YANGU KUWA HAYA TULIYONAYO NDIO MAISHA YENYEWE, HAKUNA MAISHA MENGINE ZAIDI YA HAYA TULIYONAYO KWA MAISHA YA HAPA DUNIANI.






  

VIJANA WA LEO




  Ewe kijana mwenzangu mbona unajisahau na kuzama katika dunia hii na kusahau kesho Akhera (mbinguni)? Ewe rafiki yangu mbona unazidi kumsahau mungu wako na kuzama katika mac hafu yanayo mc hukiza muumba wako eti unasema “ we go up to date (tunaenda  na wakati)” Jamani ni kweli kwenda na wakati ni kufanya matendo machafu? Unaonaje ukienda na wakati hali ya kuwa unafanya yale yaliyokuwa  mazuri yaku mfurahisha muumba?

Kijana mwezangu wakati wa ujana ndio wakati wa mitihani mingi nandio wakati wa matamanio mengi. Vijana wa leo kukicha tunaipamba miiliyetu na dunia hii kwa kwa  machafu kabisa tuna sahau kufanya vitando vizuri ambavyo vitatupatia mafanikio katika maisha yetu ya hapa duniani na kesho akhera (mbinguni). Kutokana na kuji sahau kwetu wengi miungoni mwetu tunabaki katika kilio na majuto kutokana na tabia na mienendo yetu.

Mwenyenzi mungu ametuumba wanadamu akatupa uwezo kuliko viumbe wengine. Akatupa elimu, akatupa uhuru wa kuweza kupanga na kupangua, kusuka na kufumua, kupanda na kushuka, kucheka na kulia, kuzama na kuibuka, kufunga na kufungua na mengine mengi. Pia mwenzi mungu ametujalia akili ambayo inatusaidia kupambanua mambo mbali katika maisha yetu ya kila siku.

Pamoja na mwenzi mungu kutujalia akili, pia ametujalia macho, mikono, miguu, mdomo nahivyop vingine. Basi tunapo tumia akili zetu vibaya , macho yetu kuyatumia kwa kutazama yale yaliyo haramishwa, midomo yetu tukaitumia vibaya  kama vile kutukana, kusengenya na kugonganisha watu, masikio yetu tuka yatumia kusikiliza mabo ya kipuuzi, mikono yetu tukaitumia kwa kunyang’anya na kupiga watu na miguu yetu tukaitumia kamachombo cha usafiri wa kuyaendea yale yaliyo katazwa basi tujue kuwa tutakuwa miongoni mwa watu wenye khasara.

Vijana wa leo tunavaa mavazi kinyume na tunavyo takiwa kuvaa yaani wanaume wanavaa mapambo ya kike na wanawake wanavaa nguo za kiume. Siyo hivyo tu bali mavazi yenywe hayana sifa. Kwa mfano zina kuwa fupi, zenye kubana na zinazoonesha sehemu ya ndani ya mwili (transparent).

Jambo jengine vijana wezangu ni kuhusu vijana wa kiafrika (weusi) kujibadili rangi, yaani tunaukataa uafrika (self alienation). Jamani mwenye mungu ameumba mwanadamu kwa umbo lililobora kabisa, sasa vipi tuna kataa weusi? Mbona wezetu hawajipaki masinzi iliwawe weusi kama sisi? Unafikiri wao hawaitaki rangi yetu, wao wanatami rangi yetu nyeusi lakini wanakubali na kuridhika na rangia aliyo wapa mwenyenzi mungu. Jamani kwa nini sisi tunajidharau nakutaka kuiga rangi zao?
Vijana wa kike mwenyenzi mungu amewapa nywele nzuri kabisa (nyeusi) lakini wala hawaridhiki, matokeo yake wanaamua kuweka nywele zao dawa na wengine wanaweka nywele za bandia (maiti). Lazima tuelewe kuwa kufanya hivyo tunamkashifu muumba wetu yaani tunamuona hawezi kuumba, bora tujifinyange wenyewe. Kutokana na tamaa zetu wengine wanabaki na majuto, kwa mfano hebu muangalie huyo rafiki yako jinsi alivyo utazani anaumwa kansa ya ngozi vile.
Enyi vijana wezangu tujiulize, hivi wanaume wakivaa mavazi mazuri tena ya heshima, wakaacha kuvaa mapambo ya kike kama vile heni, mikufu bangili na mengineyo na wakaacha ,kunyoa mitindo ya ajabu, hawawezi kupendeza? Kama wanaweza kupeza na kupendwa kunaumuhimu ,kuongeza mambo mengine ya karaha?
Naona vijana wa kike wakiacha kuvaa nguo za kiume.kujibadili rangi, kuvaa nguo fupi, kuweka nywele za maiti (bandia), hawawezi kupendeza ? hawawezi kupendwa? Kama watapendeza na kupendwa, je hayo mengine yana umuhimu gani?
Jamani mwanamume kuvaa mapambo ya kike kunyoa mitindo ya ajabu na kuvaa suruali za kubana wala sio dawa ya kupendeza na kupendwa, halikadhalika wanaume kuvaa nguo za kiume, kujibadili rangi, kuweka nywele za maiti (bandia) kuvaa nguo fupi na za kubana wala sio dawa ya kupendeza na kupendwa. Bali hayo yote ni kichocheo cha maovu.

Vijana wezangu mapamboa na mavazi yetu ni kero katika dunia yetu na ndio ufunguo wa zinaa. Mavazi ya kike zaidi ndio yanayo chochea dhinaa, kwani mwanamke anapovaa nguo zinazoonesha sehemu fulani huwa ni tattizo kwa wanamme, kwani kimaumbile mwanamume anaweza kushindwa kujizuiya kutokana na matamanio aliyoyapata kwa kuona sehemu fulani tu ya wawili na mwanamke. Tafadhali tumia fikra  zako na hizi ninazokupa ili ujirekebishe.



VIJANA WA LEO




  Ewe kijana mwenzangu mbona unajisahau na kuzama katika dunia hii na kusahau kesho Akhera (mbinguni)? Ewe rafiki yangu mbona unazidi kumsahau mungu wako na kuzama katika mac hafu yanayo mc hukiza muumba wako eti unasema “ we go up to date (tunaenda  na wakati)” Jamani ni kweli kwenda na wakati ni kufanya matendo machafu? Unaonaje ukienda na wakati hali ya kuwa unafanya yale yaliyokuwa  mazuri yaku mfurahisha muumba?

Kijana mwezangu wakati wa ujana ndio wakati wa mitihani mingi nandio wakati wa matamanio mengi. Vijana wa leo kukicha tunaipamba miiliyetu na dunia hii kwa kwa  machafu kabisa tuna sahau kufanya vitando vizuri ambavyo vitatupatia mafanikio katika maisha yetu ya hapa duniani na kesho akhera (mbinguni). Kutokana na kuji sahau kwetu wengi miungoni mwetu tunabaki katika kilio na majuto kutokana na tabia na mienendo yetu.

Mwenyenzi mungu ametuumba wanadamu akatupa uwezo kuliko viumbe wengine. Akatupa elimu, akatupa uhuru wa kuweza kupanga na kupangua, kusuka na kufumua, kupanda na kushuka, kucheka na kulia, kuzama na kuibuka, kufunga na kufungua na mengine mengi. Pia mwenzi mungu ametujalia akili ambayo inatusaidia kupambanua mambo mbali katika maisha yetu ya kila siku.

Pamoja na mwenzi mungu kutujalia akili, pia ametujalia macho, mikono, miguu, mdomo nahivyop vingine. Basi tunapo tumia akili zetu vibaya , macho yetu kuyatumia kwa kutazama yale yaliyo haramishwa, midomo yetu tukaitumia vibaya  kama vile kutukana, kusengenya na kugonganisha watu, masikio yetu tuka yatumia kusikiliza mabo ya kipuuzi, mikono yetu tukaitumia kwa kunyang’anya na kupiga watu na miguu yetu tukaitumia kamachombo cha usafiri wa kuyaendea yale yaliyo katazwa basi tujue kuwa tutakuwa miongoni mwa watu wenye khasara.

Vijana wa leo tunavaa mavazi kinyume na tunavyo takiwa kuvaa yaani wanaume wanavaa mapambo ya kike na wanawake wanavaa nguo za kiume. Siyo hivyo tu bali mavazi yenywe hayana sifa. Kwa mfano zina kuwa fupi, zenye kubana na zinazoonesha sehemu ya ndani ya mwili (transparent).

Jambo jengine vijana wezangu ni kuhusu vijana wa kiafrika (weusi) kujibadili rangi, yaani tunaukataa uafrika (self alienation). Jamani mwenye mungu ameumba mwanadamu kwa umbo lililobora kabisa, sasa vipi tuna kataa weusi? Mbona wezetu hawajipaki masinzi iliwawe weusi kama sisi? Unafikiri wao hawaitaki rangi yetu, wao wanatami rangi yetu nyeusi lakini wanakubali na kuridhika na rangia aliyo wapa mwenyenzi mungu. Jamani kwa nini sisi tunajidharau nakutaka kuiga rangi zao?
Vijana wa kike mwenyenzi mungu amewapa nywele nzuri kabisa (nyeusi) lakini wala hawaridhiki, matokeo yake wanaamua kuweka nywele zao dawa na wengine wanaweka nywele za bandia (maiti). Lazima tuelewe kuwa kufanya hivyo tunamkashifu muumba wetu yaani tunamuona hawezi kuumba, bora tujifinyange wenyewe. Kutokana na tamaa zetu wengine wanabaki na majuto, kwa mfano hebu muangalie huyo rafiki yako jinsi alivyo utazani anaumwa kansa ya ngozi vile.
Enyi vijana wezangu tujiulize, hivi wanaume wakivaa mavazi mazuri tena ya heshima, wakaacha kuvaa mapambo ya kike kama vile heni, mikufu bangili na mengineyo na wakaacha ,kunyoa mitindo ya ajabu, hawawezi kupendeza? Kama wanaweza kupeza na kupendwa kunaumuhimu ,kuongeza mambo mengine ya karaha?
Naona vijana wa kike wakiacha kuvaa nguo za kiume.kujibadili rangi, kuvaa nguo fupi, kuweka nywele za maiti (bandia), hawawezi kupendeza ? hawawezi kupendwa? Kama watapendeza na kupendwa, je hayo mengine yana umuhimu gani?
Jamani mwanamume kuvaa mapambo ya kike kunyoa mitindo ya ajabu na kuvaa suruali za kubana wala sio dawa ya kupendeza na kupendwa, halikadhalika wanaume kuvaa nguo za kiume, kujibadili rangi, kuweka nywele za maiti (bandia) kuvaa nguo fupi na za kubana wala sio dawa ya kupendeza na kupendwa. Bali hayo yote ni kichocheo cha maovu.

Vijana wezangu mapamboa na mavazi yetu ni kero katika dunia yetu na ndio ufunguo wa zinaa. Mavazi ya kike zaidi ndio yanayo chochea dhinaa, kwani mwanamke anapovaa nguo zinazoonesha sehemu fulani huwa ni tattizo kwa wanamme, kwani kimaumbile mwanamume anaweza kushindwa kujizuiya kutokana na matamanio aliyoyapata kwa kuona sehemu fulani tu ya wawili na mwanamke. Tafadhali tumia fikra  zako na hizi ninazokupa ili ujirekebishe.



SHEITANIMTU NI NANI?



Sheitanimtu anaweza kuwa jamaa yako, ndugu yako, rafiki yako au wewe  mwenyewe. Sheitanimtu ni kila anayeweza kumpoteza mtu akatenda jambo ovu kama vile kuiba, kuzini, kunywa pombe, kuvuta bangi na kutumia madawa ya kulevya au kukupandikiza chuki baina yako na mwengine.

Sheitanimtu kila siku unatembea naye, unakula naye lakini huwezi kumgundua kwa urahisi wakati wote unapokuwa nae hujifanya anaushari, busara  na hekima upande wako kiasi kwamba wewe mwenyewe humpenda na kumwamini kwa kumuamini na kumthamini kwako basi anajenga katika akili yako mizizi ya tabia na mwenendo wake na hivyo kukufanya uwe miongoni mwa tawi lake.

Ewe ndugu yangu sheitanimtu hafanyi mambo yake kwa siri bali hufanya kwa uwazi ili wewe uyaone na uweze kushawishika. Anaweza kunywa pombe mbele yako kutumia madawa ya kulevya, kuvuta bangi na anaweza kukusimulia jambo lolote kama uzinzi n.k vitendo na masimulizi hayo yote ni kukuvuta wewe kutoka tabia nzuri kukupeleka katika tabia mbaya.

Rafiki yangu mpendwa huyo sheitanimtu yuko tayari kutumia hata gharama ilimradi tu akupoteze. Anaweza kununua vitu vya gharama ili akupe wewe akitaka uwe tu pamoja naye katika maovu. Hapa siyo kwa jinsi yako tu, msichana anaweza kugharamiwa na mvulana au mvulana anaweza kugharamiwa na msichana kwa ajili ya kufanya uovu. Jambo hili ewe ndugu yangu ni hatari sana kwani wewe unajua fedha ni fedheha.

 Ewe ndugu yangu, wewe unaakili timamu na unajua ukweli wa mambo unajua yenye manufaa na hasara katika maisha ya kila siku. Kutokana na akili uliyokuwa nayo huna budi kuwa makini na kutafakari wakati unapopewa ushauri na huyo ambaye unasema rafiki yako. Tafadhali sana usipende kusema “ndiyo” au “hapana” bila kufikiria faida au madhara ya hiyo  NDIO AU HAPANA  yako.

Bila shaka wewe unapenda kuisha kwa amani na furaha karibu kila siku kwa hiyo huna budi  kuwa makini katika ,maisha yako. Umakini ambao ninakuambia ni “KUFIKIRI KABLA YA KUTENDA” suala hili la kufikiri kabla ya kutenda litakufanya uweze kugundua mbinu na ujanja anaotumia huyo sheitanimtu na hivyo kujiepusha naye mimi sipendi kuona wewe rafiki yangu  ukiwa katika huzuni na majuto ndio maana nina kupa mwanga katika maisha yako.

Ndugu yangu, sheitanimtu katika maisha yako ujitahidi kamuogopa kama ukoma jiepushe nae na asikuzoe nakukutawala katika akili yako na kukufanya wewe kuwa mtu usiyekuwa na kauli ya kusema HAPANA katika kila jambo la uovu.

Wewe ni rafiki na ni ndugu yangu, ninakupa mwanga huu kwa manufaa yako mwenyewe na sio kwa manufaa yangu. Nijukumu lako kutumia akili na hekima alizo kupa Mungu ili uweze kuepukana na sheitanimtu, nawe utaifanya akili yako ifanye kazi kama inavyo  takiwa. Kama ulikwisha potenzwa siyo ukate tamaa bali tumia  muda huu kujuta na kujirekebisha mara moja.

                        UJUMBE HUU UMETOLEWA NA
                        MWL: NAHONYO (FAKIHI SALUMU MSHAMU)
                                   
           







SHEITANIMTU NI NANI?



Sheitanimtu anaweza kuwa jamaa yako, ndugu yako, rafiki yako au wewe  mwenyewe. Sheitanimtu ni kila anayeweza kumpoteza mtu akatenda jambo ovu kama vile kuiba, kuzini, kunywa pombe, kuvuta bangi na kutumia madawa ya kulevya au kukupandikiza chuki baina yako na mwengine.

Sheitanimtu kila siku unatembea naye, unakula naye lakini huwezi kumgundua kwa urahisi wakati wote unapokuwa nae hujifanya anaushari, busara  na hekima upande wako kiasi kwamba wewe mwenyewe humpenda na kumwamini kwa kumuamini na kumthamini kwako basi anajenga katika akili yako mizizi ya tabia na mwenendo wake na hivyo kukufanya uwe miongoni mwa tawi lake.

Ewe ndugu yangu sheitanimtu hafanyi mambo yake kwa siri bali hufanya kwa uwazi ili wewe uyaone na uweze kushawishika. Anaweza kunywa pombe mbele yako kutumia madawa ya kulevya, kuvuta bangi na anaweza kukusimulia jambo lolote kama uzinzi n.k vitendo na masimulizi hayo yote ni kukuvuta wewe kutoka tabia nzuri kukupeleka katika tabia mbaya.

Rafiki yangu mpendwa huyo sheitanimtu yuko tayari kutumia hata gharama ilimradi tu akupoteze. Anaweza kununua vitu vya gharama ili akupe wewe akitaka uwe tu pamoja naye katika maovu. Hapa siyo kwa jinsi yako tu, msichana anaweza kugharamiwa na mvulana au mvulana anaweza kugharamiwa na msichana kwa ajili ya kufanya uovu. Jambo hili ewe ndugu yangu ni hatari sana kwani wewe unajua fedha ni fedheha.

 Ewe ndugu yangu, wewe unaakili timamu na unajua ukweli wa mambo unajua yenye manufaa na hasara katika maisha ya kila siku. Kutokana na akili uliyokuwa nayo huna budi kuwa makini na kutafakari wakati unapopewa ushauri na huyo ambaye unasema rafiki yako. Tafadhali sana usipende kusema “ndiyo” au “hapana” bila kufikiria faida au madhara ya hiyo  NDIO AU HAPANA  yako.

Bila shaka wewe unapenda kuisha kwa amani na furaha karibu kila siku kwa hiyo huna budi  kuwa makini katika ,maisha yako. Umakini ambao ninakuambia ni “KUFIKIRI KABLA YA KUTENDA” suala hili la kufikiri kabla ya kutenda litakufanya uweze kugundua mbinu na ujanja anaotumia huyo sheitanimtu na hivyo kujiepusha naye mimi sipendi kuona wewe rafiki yangu  ukiwa katika huzuni na majuto ndio maana nina kupa mwanga katika maisha yako.

Ndugu yangu, sheitanimtu katika maisha yako ujitahidi kamuogopa kama ukoma jiepushe nae na asikuzoe nakukutawala katika akili yako na kukufanya wewe kuwa mtu usiyekuwa na kauli ya kusema HAPANA katika kila jambo la uovu.

Wewe ni rafiki na ni ndugu yangu, ninakupa mwanga huu kwa manufaa yako mwenyewe na sio kwa manufaa yangu. Nijukumu lako kutumia akili na hekima alizo kupa Mungu ili uweze kuepukana na sheitanimtu, nawe utaifanya akili yako ifanye kazi kama inavyo  takiwa. Kama ulikwisha potenzwa siyo ukate tamaa bali tumia  muda huu kujuta na kujirekebisha mara moja.

                        UJUMBE HUU UMETOLEWA NA
                        MWL: NAHONYO (FAKIHI SALUMU MSHAMU)
                                   
           







Saturday, March 24, 2012

NUFAIKA / FAIDIKA NA B.M.D.E ELIMU KWA NJIA YA MASWALI NA MAJIBU

.

NAITWA ISMAILI RAMADHANI
BOX 104 KINONDONI
DAR ES SALAAM.                                         
SWALI (A)     Mara nyingi nimekuwa nikiikosa swala ya jamaa kufuatana na kioksi changu, hivyo nimekuwa nikiswalia nyumbani kwangu, hivi swala zangu hapa napata thawabu au vipi?

SWALI(B)      Nilivyosoma mimi katika lugha ya kiarabu neno jamaa huanzia na watu au vitu vitatu, hivi tunaposema swala ya jamaa, inamaanisha inaanzia na mtu mmoja au watatu kama nilivyo soma mimi? naomba nifahamisheni.

JIBU(A)   Kwanza ifahamike vema kuwa swala ya jamaa ni fardhi kifaayat (nguzo) kama ilivyo swala jenaiza yameelezwa hayo katika vitabu vitu vya sheria na walimu wanatufunza jambo hilo kila siku, nalengo kuu ya swala ya jamaa nikuleta muungano kwa waislamu (unity) na kuondoa kabisa mtengano (veriety) nazimepokelewa hadidhi nyingi tu juu ya kuhimizwa swala ya jamaa, mimi nanza na hii :- amesema mtume mtukufu (saw) kwamba, laukama watu wangejua ubora naladhima zilizopo katika swala ya jamaa basi wangelileta hata kwa kutambaa (kama wangekuwa ni vilema) hapa mtume mtukufu (saw) anahimiza swala ya jamaa (hata kama mtu angekuwa kilema hana miguu)
FADHILA ZA SWALA YA JAMAA.
Amesema mtume mtukufu (saw) kwamba: swala ya  jamaa inaizidi fadhila swala ya mwenye kuswali pekeyake kwa madaraja ishirini na saba na katika mapokezi mengine katika hadidhi sahihi kabisa aliyoipokea imamu Bukhary kutoka kwa mtume mtukufu (saw) amesema swala ya mtu katika jamaa inaizidi swala yake yakuswalia nyumbani au sokoni kwake mara ishirini na tano (25) hii ni kwa ajili ya hatua anazotumia mtu huyo kwa ajili ya mola wake.

Hivyo shughuli zetu zisitutawaler mpaka tukaacha swala ya jamaa, tazama swahaba huyu aliyekuwa kipofu Abdallah bin ummimaktuum alivyokatazwa kuswalia nyumbani pamoja na tatizo lake la upofu. Hii ni pale alipo mjia mtume mtukufu (saw) kasha akamwambia hivi:-

Ewe mtume mimi nikipofu na usiku ni kiza njiani kuna mashimo, je unaweza kunipa ruksa ya kuswali nyumbani swala ya isha na alfajiri kufuatana na tatizo langu la upofu mtume alijibu hivi; sikupi ruksa hata kidogo kwa ajili ya ubora na umuhimu wa swala ya jamaa.

Tazama huyu ni kipofu amenyimwa amenyimwa ruksa ya kuswalia nyumbani je sisi wenye macho ingekuwa vipi?
Pia mtume mtukufu (saw) alipata kusema hivi:- namuapia muenyenzi mungu ambaye nafsi yangu imumikononi mwake, kwa hakika nimekusudia kuamrisha zikatwe kuni halafu uwashwe moto, kasha niwaamrisha watu kuswali kasha itolewe adhana ,kasha nimrishe mtu awaongeze watu, kasha nitoke niwaendee watu wanayo ikhalifu swala ya jamaa nikawaunguzie manyumba yao kwa kosa hilo ( lakuhacha jamaa) .
Hii hadidhi sahihi kabisa inayowahimiza watu waswali swala ya jamaa, wasiache pamoja na kuwa uwezo wa kuetekeleza. Hivyo fahamu kazi kuwa swali ya jamaa ni fardhi kifaayat kwa mtu mkazi isipokuwa kwa msafiri ni suna muakadat hata lazimika kuiswali.

JIBU (B)         Neno jamaa kisheria katika swala huanzia na watu wawili imamu na maamuna nakuendelea……….
Na kilugha huanzia na watu watatu au vitu vitatu na kuendelea……………
Naswalaa ya jamaa huwakusanya wanaume na wanawake pia.
            FAIDAT WAFURUU SHARIAT.
Mwanaume unapo swalia nyumbani anapata daraja moja na anapo swalia jamaa kama msikitini kama upo anapata daraja ishirini na saba.
Mwanamke anapo swalia nyumbani anapata daraja ishirini na saba na anapo swalia msikitini anapata daraja moja.
                                    Walaahu aalamu.