Wednesday, February 12, 2020

TIBA YA KIFUA NA PUMU HATA KAMA NI SUGU.
chukua binzari shomari, mdalasini, a rkisusi, habbat Sauda, zaatar, khaulinjan na lisaan uswfuur, ziponde kisha ziloweke kwenye maji Lita moja na nusu ichemshe mpaka ibaki Lita moja

Matumizi
Mtoto mchanga kijiko cha chai Mara 3, mtoto wa mwaka 1-3 kijiko cha chakula Mara 3, mtoto miaka 8-12 kikombe cha kahawa Mara 3, waliojuu ya miaka 12 robo kikombe cha chain. Kwa mda wa siku 21.       
 DAWA YA MAFUA ISIYO NA MADHARA

Watu wengi husumbuliwa sana na mafua makali na wakati mwingine kupiga chafya mfululizo.

 Ili kuondokana na tatizo la mafua unashauriwa kuandaa kinywaji kifuatacho kisicho na kemikali.

MAANDALIZI

Chukua :

1. Maji lita moja

2. Asali vijiko 3 vikubwa vya chakula

3. Tangawizi ya unga kijiko kimoja kikubwa cha chakula au tangawizi mbichi itwange upate mchanganyiko uliopondeka kijiko kimoja kilichojaa.

Chemsha mchangyanyiko wako wote huo kwa pamoja mpaka uchemke vizuri ambapo inategemea na moto wa jiko lako lakini mpaka utakapoona imechemka vizuri usiache ikakaukia jikoni inashauriwa dakika 15 hadi 20 inatosha.

Kisha iache ipoe na KUNYWA NUSU GLASI MARA TATU kwa siku yaani asubuhi , mchana na usiku.

 Kwa wale walio na mafua sugu yanadondoka muda wote na kupiga chafya nyingi sana zisizo na idadi basi zitakata mara moja na siku ya pili zitaisha kabisa kumbuka kunywa dawa hii mwezi mzima au hadi miezi miwili utapona kabisa.

Kinywaji hiki ni dawa ya mafua safi kabisa unatumia siku moja tu unakua na nafuu kabisa ila dozi yake inataka utumie mwezi mmoja hadi mwezi mmoja na nusu mfululizo bila ya kuacha.
Hata ukiona umepoa endelea kutumia kwani Hii ni itakusaidia hata kwa maradhi mengine na kuepuka mafua kuja mara kwa mara