Shukrani zisizo na kikomo ni zake Allah, Muumba na mlinzi wa viumbe wote. Rehema na amani zishuke kwake Mtume Muhammad(s.a.w) na watu wake wote pamoja na maswahaba wake.
Ndoa ni lazima/wajibu kwa mtu ambaye hawezi kujizuia na ZINAA na akawa ni mwenye uwezo juu ya MAHARI na matumizi (mahitaj /huduma) kwa mke. Katika ndoa MAHARI ni kitu cha lazima kwa jina jingine huitwa SADAKA, hii ni mali anayotoa mume kumpa mke na wala si wazazi au jamaa wa mke bali ni yake mwenyewe mwanamke. Lakini mke anaweza kuamua kwa hisani yake mwenyewe kuwapa wazazi wake au kwenda kutumia na mume wake. Wazazi na jamaa kupanga kiasi cha MAHARI na kutumia bila kumshirikisha binti mwenyewe ni makosa makubwa ndugu zangu.
Makosa mengine tunayofanya ni kutoza MAHARI kubwa, jambo hili linapelekea wanaume waliowengi washindwe kuona kwasababu ya kukosa uwezo na hatimaye wanaendelea na maasi ya ZINAA na wale wanaobahatika kuoa kwa MAHARI hiyo kubwa wanabaki hata hawana kianzio katika maisha yao ya ndoa. MAHARI haina kikomo/ mpaka kwa uchache au wingi wake lakini kinacho takiwa MAHARI hiyo iwe na manufaa na thamani , Mtume (S.A;W) juu ya hili anasema "TOENI ANGALAU PETE YA CHUMA"
Katika kuchumbia ni SUNNA kwa mume kutazama uso na viganja vya mchumba wake na wakati wa kutazama awapo ndungu wa mke, juu la hili mtume anasema "ATAKAPOCHUMBIA MMOJA WENU MWANAMKE AKIWEZA KUYATAZAMA YALE YATAKAYO MPELEKEA KUMUOWA KWAKE BASI AFANYE". Hapa tunaambiwa kutazama uso na viganja vyake na wala si kufanya nae ZINAA ati tunafanya majaribio (practical ) majaribio. kufanya hivyo kabla ya ndoa ni makosa makubwa na hukumu yake ni kuchapa BAKORA MIA (100). kwa Mume na Mke, kwa vile ni wazinifu.
Ndoa ya kiislam ili iswihi /ikubalike ni lazima awepo Mlezi /Msaidizi na mashahidi wawili waislamu waliowaadilifu, Waliohuru na wawe wanaume (kwa pande zote mbili ). Juu ya hili Mtume (S.A.W) anasema MASHAIDI WAADILIFU". Sasa je, Ndoa hizo za mkeka hao wote wanakuwepo? kama wanakosekana uhalali unatoka wapi?
Enyi ndugu zangu, ni haramu /haitakiwi kwa muislamu kumuoa au kuolewa na asiye kuwa muislamu na vilevile ni haramu kuolewa au kumuoa ndugu yako kwa ukaribu wa ukoo au KUNYONYA au UKWE au kuwachanganya ndugu pamoja (yaani mkumbwa na mdogo au mapacha kuwaoa wote kwa pamoja kama wafanyavyo wengine).
Enyi ndugu zangu mliokili upweke na utukufu wa Allah, hivi jinsi tunavyosherekea ndoa zetu ndivyo inavyotakiwa katika ndoa, tunaweka Mikesha ambayo inaambatana na muziki na pengine na pombe. jamani ndiyo ni furaha lakini mnaonaje furaha hiyo tujisherekea kwa kusoma Quran, kupeana mawaidha, kusoma riwaya za Mtume (S.A.W). kuburudika kwa Qaswida na pengine hata kwa Dhiki?.
Kumbuka: "MJNGA NCHI NI MWANANCHI" na "MJENGA DINI NI MWANADINI (MUUMINI)". Kwa hiyo basi tufanye mambo yanayoendeleza dini na wala si yale yanayopunguza thamani ya dini. Ndoa ni jambo la furaha na Kheri kwa hiyo tutumie nafasi hiyo kuomba dua ili Allah alete mafanikio katika ndoa badala ya kuweka kanda za muziki tuweke kanda za dini. tuzinduke zangu ili tufanikiwe hapa Duiniani na kesho Akhera.
Kwa leo namalizia kwa maneno ya kiongozi watu Mtume (S.A.W) pale aliposema "MTU MWENYE KUWEZA MIONGONI MWENU KUOA BASI AOE HAKIKA LINASITIRI JICHO NA NI KINGA YA UTUPU NA ASIYEWEZA (KUOA ) BASI NI JUU YAKE KUFUNGA"
"MWENYEZI MUNGU NA MTUME WAKE NDIO WANAOJUA KULIKO MIMI NA WEWE.
SALAMU HIZI ZIMETOLEWA NAMI MCHACHE WA ELIMU.
MWL. NAHONYO (FASANA)
Ndoa ni lazima/wajibu kwa mtu ambaye hawezi kujizuia na ZINAA na akawa ni mwenye uwezo juu ya MAHARI na matumizi (mahitaj /huduma) kwa mke. Katika ndoa MAHARI ni kitu cha lazima kwa jina jingine huitwa SADAKA, hii ni mali anayotoa mume kumpa mke na wala si wazazi au jamaa wa mke bali ni yake mwenyewe mwanamke. Lakini mke anaweza kuamua kwa hisani yake mwenyewe kuwapa wazazi wake au kwenda kutumia na mume wake. Wazazi na jamaa kupanga kiasi cha MAHARI na kutumia bila kumshirikisha binti mwenyewe ni makosa makubwa ndugu zangu.
Makosa mengine tunayofanya ni kutoza MAHARI kubwa, jambo hili linapelekea wanaume waliowengi washindwe kuona kwasababu ya kukosa uwezo na hatimaye wanaendelea na maasi ya ZINAA na wale wanaobahatika kuoa kwa MAHARI hiyo kubwa wanabaki hata hawana kianzio katika maisha yao ya ndoa. MAHARI haina kikomo/ mpaka kwa uchache au wingi wake lakini kinacho takiwa MAHARI hiyo iwe na manufaa na thamani , Mtume (S.A;W) juu ya hili anasema "TOENI ANGALAU PETE YA CHUMA"
Katika kuchumbia ni SUNNA kwa mume kutazama uso na viganja vya mchumba wake na wakati wa kutazama awapo ndungu wa mke, juu la hili mtume anasema "ATAKAPOCHUMBIA MMOJA WENU MWANAMKE AKIWEZA KUYATAZAMA YALE YATAKAYO MPELEKEA KUMUOWA KWAKE BASI AFANYE". Hapa tunaambiwa kutazama uso na viganja vyake na wala si kufanya nae ZINAA ati tunafanya majaribio (practical ) majaribio. kufanya hivyo kabla ya ndoa ni makosa makubwa na hukumu yake ni kuchapa BAKORA MIA (100). kwa Mume na Mke, kwa vile ni wazinifu.
Ndoa ya kiislam ili iswihi /ikubalike ni lazima awepo Mlezi /Msaidizi na mashahidi wawili waislamu waliowaadilifu, Waliohuru na wawe wanaume (kwa pande zote mbili ). Juu ya hili Mtume (S.A.W) anasema MASHAIDI WAADILIFU". Sasa je, Ndoa hizo za mkeka hao wote wanakuwepo? kama wanakosekana uhalali unatoka wapi?
Enyi ndugu zangu, ni haramu /haitakiwi kwa muislamu kumuoa au kuolewa na asiye kuwa muislamu na vilevile ni haramu kuolewa au kumuoa ndugu yako kwa ukaribu wa ukoo au KUNYONYA au UKWE au kuwachanganya ndugu pamoja (yaani mkumbwa na mdogo au mapacha kuwaoa wote kwa pamoja kama wafanyavyo wengine).
Enyi ndugu zangu mliokili upweke na utukufu wa Allah, hivi jinsi tunavyosherekea ndoa zetu ndivyo inavyotakiwa katika ndoa, tunaweka Mikesha ambayo inaambatana na muziki na pengine na pombe. jamani ndiyo ni furaha lakini mnaonaje furaha hiyo tujisherekea kwa kusoma Quran, kupeana mawaidha, kusoma riwaya za Mtume (S.A.W). kuburudika kwa Qaswida na pengine hata kwa Dhiki?.
Kumbuka: "MJNGA NCHI NI MWANANCHI" na "MJENGA DINI NI MWANADINI (MUUMINI)". Kwa hiyo basi tufanye mambo yanayoendeleza dini na wala si yale yanayopunguza thamani ya dini. Ndoa ni jambo la furaha na Kheri kwa hiyo tutumie nafasi hiyo kuomba dua ili Allah alete mafanikio katika ndoa badala ya kuweka kanda za muziki tuweke kanda za dini. tuzinduke zangu ili tufanikiwe hapa Duiniani na kesho Akhera.
Kwa leo namalizia kwa maneno ya kiongozi watu Mtume (S.A.W) pale aliposema "MTU MWENYE KUWEZA MIONGONI MWENU KUOA BASI AOE HAKIKA LINASITIRI JICHO NA NI KINGA YA UTUPU NA ASIYEWEZA (KUOA ) BASI NI JUU YAKE KUFUNGA"
"MWENYEZI MUNGU NA MTUME WAKE NDIO WANAOJUA KULIKO MIMI NA WEWE.
SALAMU HIZI ZIMETOLEWA NAMI MCHACHE WA ELIMU.
MWL. NAHONYO (FASANA)