Friday, June 5, 2015

MFAHAMU FAKIHI SALUMU MSHAMU (MWL. NAHONYO)

Huyu ni mwalimu kitaaluma aliyefikia chuo kikuu. Huyu ni mtoto wa Mzee Salumu Mshamu na Bi Esha Namalove wa Mtongwele Chilangala wilayani Newala.
Alizaliwa tarehe 01/05/1980 katika kijiji cha Mtongwele Chilangala, mwaka 1989-  1995 alisoma elimu ya msingi katika shule ya msingi Mbonde wilayani Newala.
Mwaka 1996 -  1999 alisoma elimu ya sekondari katika shule ya sekondari ya kutwa Mnyambe wilayani Newala.
Mwaka 2003 alijiunga na mafunzo ya ualimu katika chuo cha ualimu Bustani wilayani Kondoa mkoani Dodoma kwa ngazi ya cheti.
Mwaka 2004 aliajiriwa na Halmashauri ya Wilaya kama mwalimu wa shule ya msingi Mbonde.
Mwaka 2010 alifanya mtihani wa kidato cha sita kama mtahiniwa wa kujitegemea, baada ya matokeo alijiunga na chuo kikuu cha waislam Morogoro kwa ajili ya shahada ya ualimu ambapo mwaka 2013 alihitimu na kutunukiwa shahada.

TUNU ALIYOJALIWA; NGAZI ZOTE ZA UALIMU ALIZOPITIA AMEWAHI KUWA KIONGOZI. MAASHAALLAH

No comments:

Post a Comment