Saturday, July 4, 2015

NIUNGENI MKONO WANANEWALA WOTE

Namshukuru Mwenyezi Mungu muummba wa mbingu na ardhi na vilivyomo humo na vilivyo baina ya mbingu na ardhi. Ninania ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge katika jimbo jipya la Newala Vijijini tukijaliwa kupata jimbo na kama vigezo havitakidh i vya kupata jimbo basi inshaallah nitagombea jimbo la Newala natarajia kupitia Chama cha Mapinduzi.

Ombi langu kubwa kwenu wadau wa blog hii  na WanaNewala mniunge mkono kwania yangu hii. Naingia nikiwa najua kuwa ninadhima kubwa ya kurudisha matumaini kwa wanainchi waliokosa imani kwa chama cha mapinduzi na serikali yake, vilevile najua kuwa kuna makundi hayajaguswa kabisa.

Ninania  ya dhati kabisa naomba mniunge mkono kwa hali na mali ,  kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tunaweza kutatua changamoto mbalimbali zinazotukabili Wananewala inshaallah. Changamoto  za Newala wala hazihitaji elimu ya chuo kikuu kuweza kuzibaini au kuzitatua bali zinahitaji umoja, mshikamano na uongozi madhubuti chini ya Fakihi Mshamu kama Mbunge mtarajiwa wa Jimbo jipya la\ Newala.

Wadau wenzangu wa Newala, kumbukeni  kuwa mageuzi ya aina yeyote yanahitaji  mambo makuu mawili; wakati  na umoja. Ni matumaini yangu kuwa wakati umekwishafika kilichobaki ni ninyi kuungana nami na kuunda umoja ili tulete mageuzi. Nakuja kwenu nikijua kuwa HAYA TULIYONAYO NDIO MAISHA YENYEWE NA HAKUNA MAISHA MENGINE ZAIDI YA HAYA TULIYONAYO KWA HAPA  DUNIANI NA KILA AHADI NI  YENYE  KUULIZWA  MBELE  YA MWENYEZI MUNGU.

Tunayo  mengi yenye tija kwa  ustawi wa Wananewala, wakati ukifika tutawaelezeni  na tutawaomba mtuunge mkono. WITO WANGU  KWENU NI KUWA MAKINI  NA  WAGOMBEA  WATAKAOJARIBU  KUZINUNUA AKILI  ZENU ILI MSIFANYE CHAGUO  SAHIHI, KUMBUKENI KUWA MIAKA MITANO NI MINGI SANA ENDAPO MTAKUWA KATIKA SHIDA  NA  M ANUNG'UNIKO  NA NI MICHACHE ENDAPO MTAKUWA KATIKA FARAJA NA FURAHA, AKILI YAKO  NDIO  DHAMANA  YAKO.

No comments:

Post a Comment