Thursday, November 17, 2011

KILA MUISLAMU ANDHIMA YA KUENDELEZA UISALAMU.

Shukrani  zilizo takasika ni zake Allah (s.w.t) asiyekuwa na mshirika katika  Ibada yake  wala katika  ufalme  wake.
Rehema na Amani zishuke juu ya Mtume Muhammad (s.a.w) na wale wote wenye kushikamana naye.
Mwenyezi Mungu ametujaalia wanadamu kuwa makundi mbali mbali  kama vile  masikini  na  matajiri, wafanya  kazi  na  wakulima  na  makundi  mengine  mengi. Pamoja na  kuwepo na  makundi  mbali  mbali  kila  kundi  linatakiwa  kumcha  Allah (s.w.t) na kuwa msari wa  mbele  katika  kuendeleza  dini.
Wewe na mimi  tumetamka shahada mbili  na tumekirir katika nyoyo zetu kuwa mwenye jina la Allah ndiye  mungu wa  kweli  na Muhammad ni Mtume wake, kukiri na kutamka shahada ni dalili tu ya kujulisha  kuwa sisi ni waislamu. Ili uislamu wetu uweze kukamilika  tunatakiwa  kuyafanya  yale ametuagiza Allah (s.w.t.) na Mtume wake na kuyaacha yale ambayo wametukakaza.
Katika  makundi tuliyonayo wanadamu  kundi la wafanya  kazi huwa wamepitia  hatua mbali  mbali kama vile shule ya msingi, sekondari, chuoni na  hatimaye kazini. Sasa ewe uliye jaaliwa muajiriwa ujiulize  ukiwa shule  ya  msingi, sekondari na chuoni, mlianza wangapi, mlifaulu  wangapi na mpaka hivi sasa ni wa ngapi mnaendelea na kazi?
Je wale ambao hawaku fanikiwa katika yale maeneo ambayo wewe umefanikiwa unafikiri ni uzembe wao  au Allah hakuwawezesha? Na wew uliye fanikiwa unafikiri umefanikiwa kwa ujanja wako au Allah ndiye aliyekuwezesha?
Allah (s.w.t) humpa amtakaye na humnyima amtakaye, umekuwa miongoni mwa waliopewa na Allah basi nawe utowe katika njia ya Allah ili kuendeleza dini yake si kwaajili ya kumnufaisha mwenyezi mungu bali ni kwaajili ya kutaka radhi ili aendelee kukuruzuku na kulinda  mali  yako.
Mwenyezi Mungu anatuhimiza kwa kusema ndani ya Quran: ENYI MLIOAMINI TOENI KATIKA VILE TULIVYOKUPENI KABLA HAIJA FIKA SIKU AMBAYO HAPATAKUWA (NA) WALA URAFIKI (WA KUSAIDIANA) WALA UOMBEZI, NA WALIOKUFURU NDIO WALIO JIDHULUMU (KWELIKWELI) Q:2:254.    
Allah (s.w.t.) ametuambia wanadamu atatupa uwezo kuliko viumbe wote, ametupa elimu, akatupa pia uhuru wa kuweza kupanga na kupangua,  kutanda na  kutandua, kufunga  na kufungua  na mengine  mengi.  Tujiulize  enyi wenzangu, katika kipato  chetu  tunatumia kiasi  gani  katika  mabo  ya anasa?
Kwanini tunakunja mikono yetu katika upnde wa kundeleza dini yetu?
Sisi tuliojaaliwa kuwa na uhakika wa kupata tena kwa muda maalumu tunakuwa wazito wakutoa je, wale wasio kuwa na uhakika wa kipato kwa muda maalumu wataweza? Waislamu wenyewe tusipo iendeleza dini yetu asiye kuwa Muislamu ataweza kuundeleza Uislamu?
Allah (s.w.t) amemsifu binaadamu kwa kusema “ HAKIKA TUMEMUUMBA MWANAADAMU KATIKA UMBO LILILO BORA KABISA” 95:4. Hapa inamaana wewe na mimi tumejaliwa  vipawa  vinavyoweza kutuwezesha kutambua dhima ya kuumbwa kwetu na hatima ya maisha yetu hapa duniani na kesho akhera.
Enyi ndugu zangu katika imani na din tujitahidi kutoa bila kuwa na mashaka ya kulipwa katika vile tunavyovitoa, Allah  ameahidi kumlipa lika mtu kwa kila akifanyacho kiwe ch kheri au shari, kidogo au kikubwa, akiwa ametoa kwa siri au wazi kama navyo sema ndani ya Quran 2:274 “WALE WANAOTOA MALI ZAO USIKU NA MCHANA KWASIRI NA DHAHIRI, WANAUJIRA WAO KWA MOLA WAO, WALA HAITAKUWA KHOFU JUU YAO  WALA H WATA HUZUNIKA”
Ewe Mwenyezi Mungu , kila atakaye kunjua  mkono wake na kutoa kwako basi mtengenezee mambo yake hapa Duniani na Kesho Akhera.

No comments:

Post a Comment